waptrick.com

Waptrick Lady Jay Dee - Teja Song Lyrics


Waweza Kuwa kituko, Ugeuke kichekesho

Wakati mtu mzuri, Penzi likakubadili

Sumu nilioimeza, Sijui ni sumu gani

Nimefanya naloweza, Na bado ni taabani

Nimeshakunywa maziwa, Sumu sijaitapika

Akili haifikiri, Nimekumbwa kitu gani

Nina zunguka zunguka, Ninatembea tembea

Ninaongea ongea, Na hata sijielewi

Au nimekuwa teja, teja wa mapenzi

Oooh Nimebwia unga , ooh sijiweza

Mimi nimekuwa teja, teja wa mapenzi

Huu nilobwia unga, sijui aina gani

Kumbe mapenzi ni sumu, kumbe mapenzi uteja

Hasa yakiwa magumu, unageuka kioja

Na mimi sijifahamu, nimeenda kila rehab

Nikipona narudia, na kuyaacha nimeshindwa

Nina zunguka zunguka, ninatembea tembea

Ninaongea ongea, na hata sijielewi

Mimi nimekuwa teja, teja wa mapenzi

Oooh nimebwia unga , ooh sijiwezi

Mimi nimekuwa teja, teja wa mapenzi

Huu nilobwia unga, sijui aina gani

Nilidhani natafuta faraja, na kumbe nina anguka (kwenye uteja)

Zungu linipa maradhi iiiiiiiih iiih, maradhi

Na bado nalizimia, tena sana

Pesa zenyewe hakuna, Na bado nakimbilia

Kumbe mapenzi uteja, uteja

Kumbe nimekuwa teja , teja wa mapenzi

Jamani nimebwia unga, ooh sijiwezi

Mwenzenu nimekuwa teja, teja wa mapenzi

Sijui nilobwia unga, sijui aina gani

Teja ni hoi taabani, teja wa mapenzi

Teja ni hoi kitandani , oooh sijiwezi

Kumbe nimekuwa teeeja, teja wa mapenzi

Kumbe nimekuwa teja aah, Sijui aina gani

----
» Lady Jay Dee other songs
« Lyrics Search
« Waptrick Home Page
« Change Language
» Download free VPN for iPhone