Chorus
Mnakula kunywa na kuvaa, siku zinaendaa
Vya bure hupenda kupewa, wala hamna fikira
Kila upande mnafiti, siku zinaenda
Vinywa vimejaa ufitini, wanaume kama mabinti
Verse 1 -
Lady Jaydee
Ninavyosema wanaume simaanishi woteella wale ye tabia kama za mabinti
Utawaona kwenye magari ya mademu zao
Wakitanua na kucheka, utadhani yao
Hupenda kuwaliwaza wamama, watu wazima
Hawana mapenzi ya kweli, moyoni wanawaza pesa
Nikisema wanajiuza, katu sitokosea
Tutawatofautishaje hawa na machangudoa
Repeat Chorus
Verse 2 -
A-Y
Sema sema sema, haki yako Jaydee
Tembo kuvaa vipusa, haki yako ni halali zaidi
Siwezi danganya, sina upendo upande mlipo marafiki
Ndugu aa mwisho wa wiki, hatuwezi kuwa washkaji
Kama una moyo wa plastik, Ambwene aliona
Usoni kama watu, mioyoni unafiki mtupu
Siyo kula siyo kuvaa tegemezi mpaka mkwanja wa kondomu
Sikufahamu hii ni simple zaidi ya kumnyatia kiziwi
Wanaume gani hawaelewi mambo ya kiume
Nataka muache kutazama, nataka muone
Mnajidanganya wenyewe na inakolea zaidi ya mnapodanganya wengine
Sizuii msifanye mfanyayo
Tunafikiria kwa ubongo, siyo kwa nyayo
Inshaalla inshaalla kibao maisha kuwafuata mbio
Ujinga huo kusanya mawazo yenu na ninaacha mungu awahukumu
Binamu
Repeat Chorus
Verse 3 -
Lady Jaydee
Ukiwakuta kwenye vikao vya pombe
Eti wao wasemaji wanaojua yote
Kumbe hatoi hata senti ya kulipa bili
Ikifika zamu yao huenda msalani
Kwa ukuwadi wao namba moja hupenda
Wanapenda kuwaliwaza mademu wa wenzao
Shoga zangu hebu leteni magauni tuwavishe
Hijabu tuwafunge na vimini vitopu tuwaazime
Repeat Chorus
Verse 4
Umeona wapi
Wanaume kunyweshwa pombe
Hivi tangu lini dume likasutwa
Umesikia ya jana
Hassan naye kaja Kitchen Party
Mwanishangaza!
Repeat Chorus
----